Lukaku akataa kandarasi ya £140,000 kwa wiki Everton

Mshambuliaji wa Uhispania na Chelsea Diego Costa, 28, anataka kuondoka Stamford Bridge kwa wakati anaotaka yeye, na jambo hilo linachelewesha hatua ya Chelsea kumsajili Romelu Lukaku, 24, kutoka Everton (Daily Mirror).
Antonio Conte anataka Chelsea watoe hata pauni milioni 100 kumsajili Romelu Lukaku, kama Everton wanataka kiasi hicho ili kumuuza (The Telegraph).
Mshambuliaji kutoka Argentina Lionel Messi, 30, atasaini mkataba mpya Barcelona mara tu atakaporejea kutoka kwenye fungate yake baadaye mwezi huu (Goal).
Paris Saint-Germain wanajiandaa kupanda dau jipya la kumtaka mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, na wamewasiliana na wawakilishi wa mchezaji huyo (L'Equipe).
Arsenal wanapanga kutoa pauni milioni 70 kuwasajili viungo wawili kutoka Sporting Lisbon ya Ureno, William Carvahlo, 25, na Gelson Martins, 22 (A Bola).

No comments

Powered by Blogger.